Otile Brown ft Barakah the Prince – Umenipendea nini Lyrics
Check out “Umenipendea Nini” lyrics by Otile Brown, featuring Barakah the Prince on Kelxfy. “Umenipendea Nini” is off Otile Brown’s new album, “Grace“.
Umenipendea Nini Lyrics
Yeah! Teta design ya maneno
Kushawishi moyo
Yalivyonitenda mapenzi
Kuyakurupukia tena, siwezi
Kidogo initoe uhai
Usione nakuringia
Nayaogopa mapenzi
Mapenzi hayajakamilika
Mapenzi ni maridhiano
Imani na nia
Mapenzi ni mawasiliano
Nami nina maswali mengi kwako
Kilichokutenganisha na ex wako
Usiseme unanipenda
Na hujamaanisha
Hivi, umenipendea nini?
Sema umenipendea nini?
Sema basi umenipendea nini?
Sema umenipendea nini?
(Ihaji Made It)
Mmmh! Na sio sina mapenzi
Ila mapenzi yalinitia kiburi
Yalichonitenda enzi hizooo
Maana, wengi niliwapa mapenzi
Baada ya penzi nikavuna uadui
Naogopa mwisho vilio
Mapenzi hayajakamilika
Mapenzi ni maridhiano (Ni maridhiano)
Imani na nia
Mapenzi ni mawasiliano
Nami nina maswali mengi kwako
Kilichokutenganisha na ex wako
Na kama wanipenda
Na hujamaanisha
Hivi, umenipendea nini?
Sema umenipendea nini?
Sema basi umenipendea nini?
Niambie umenipendea nini?
Mimi umenipendea nini?